Chimbuko la Ukoo = KAUKI

Chimbuko la Ukoo = KAUKI
KAUKI

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)
TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA 14 WA KAUKI

Jumapili, 14 Aprili 2024

KAMATI ZA MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU WA 13 WA KAUKI


 

UONGOZI WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI) WAWAKUMBUSHA WANAUKOO KUHUSU MKUTANO MKUU


Viongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) kwa niaba ya Wanaukoo Wote; wanayofuraha kubwa kuwakumbusha kuwa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI unatarajia kufanyika Siku ya Jumamosi ya tarehe 29 Juni 2024, Kijijini Kidamali, Mkoa wa Iringa. Mkutano huu ni Mwendelezo wa Mikutano ya Ukoo ambayo hufanyika kila Mwaka.

Ili kufanikisha Mkutano huo, Wanaukoo Wote wanaombwa kutoa Michango yao ili kufanikisha Mkutano huo. Watu Wazima Watachangia Shilingi 10,000/- na Watoto 5,000/-. Michango hii itasaidia upatikanaji wa huduma za Chakula, Chai na Maji kwa Siku zote tutakazokuwa Kidamali. Michango itolewe kwa Viongozi wa Kanda Husika.

 Malengo ya Mkutano Mkuu ni pamoja na:

1.     Kutambulishana na Kufahamiana Ndugu/Wanaukoo;

2.     Kujua Chimbuko na Historia ya Ukoo wa Kivenule;

3.     Kubadilishana Taarifa na Uzoefu Mbalimbali wa Shughuli za Maisha;

4.     Kuweka mikakati mbalimbali ya kuimarisha undugu na ushirikiano baina ya Wanaukoo; na mengineyo.

Mikutano ya KAUKI huhudhuriwa na Wanaukoo kutoka Maeneo ya Magubike, Kidamali, Kalenga, Nzihi, Nyamihuu, Nyamahana, Nduli, Mgongo, Itagutwa, Igominyi, Vilalo, Migoli, Iringa Mjini, Mafinga, Dar es Salaam, Morogoro, Mwanza na Maeneo mengine ambayo washiriki wanaishi.

 Imeandaliwa na Kutolewa na:


Uongozi wa KAUKI

 

Sambaza kwa Ndugu Wote.

MKUTANO MKUU WA 13 WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)


 

Ijumaa, 27 Oktoba 2023

CHIMBUKO NA MUUNDO WA UKOO WA KIVENULE - KAUKI






VIONGOZI WA KAUKI WASISITIZA UMUHIMU WA KUSHIRIKI KATIKA MISIBA YA NDUGU/WANAUKOO

 

Viongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) walifanya mazungumzo kuhusu umuhimu wa ndugu/wanaukoo kushirikiana katika misiba na raha. Katika mazungumzo hayo, Mwenyekiti wa Ukoo wa Kivenule Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule alielezea kuhusu taratibu zinazotumika maeneo mbalimbali kuhusu uratibu na ushiriki katika misiba ya ndugu/wanaukoo.


Mwenyekiti alifafanua kuwa jukumu la kuratibu, kushiriki na kusimamia shughuli za misiba hubebwa na ndugu/wanaukoo waliopo katika eneo ambalo msiba unakuwa umetokea. Ndugu/Wanaukoo toka maeneo mengine, jukumu lao ni kusaidia kufanikisha shughuli za msiba huo. Kwa muktadha huo, hata viwango vya ushiriki katika msiba husika hutofautiana na wahusika waliopo eneo ambako kuna msiba. Lakini bado wajibu wa kuhakikisha shughuli zinazohusiana na msiba zinafanikiwa ni za kila ndugu/mwanaukoo.

Jambo la muhimu kuzingatia ni ushiriki wa ndugu/wanaukoo katika matukio yote ya misiba ya ndugu/wanaukoo; tofauti inayokuwepo ni viwango vya michango ya rambirambi ili kuweza kufanikisha mazishi ya msiba husika.

Kila maeneo wanatenga viwango vya michango ya rambirambi kwa msiba unaokuwa umetokea katika eneo husika. Pia kuna viwango vya michango kwa ajili ya misiba ambayo inakuwa imetokea mbali na maeneo ambayo msiba unakuwa unakuwa umetokea.

Basi tunasisitiza kuwa ni lazima tushiriki katika misiba yote, ila viwango vitatofautiana kwa misiba ambayo inakuwa imetokea maeneo yetu tunayoishi na ile ambayo imetokea maeneo ambayo hatuishi, lakini tuna wajibu wa kushiriki kwa hali na mali.

Hii itasaidia kupunguza mzigo wa michango kwa sababu kuna wakati kunakuwa na mfululizo wa misiba…kitu ambacho kinaweza kuwafanya ndugu washindwe kumudu.

Kwa hiyo, tunaweza kupendekeza viwango vya michango kwa misiba iliyotokea maeneo ya mbalimbali na tunapaswa kutoa rambirambi zetu.

Kwa ndugu wote tunaoishi Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Mafinga, Mwanza na maeneo mengine tunapaswa kutoa rambirambi kwa msiba uliotokea Magubike. Tutoe chochote kwa kadri Mungu atakavyokuwa ametujalia.

Suala la Jingine lilikuwa kwenye mjadala ni ushiriki wa misiba kwa ndugu/wanaukoo. Tulilizungumzia suala la ndugu wengi waliopo Dar es Salaam na maeneo mengine tofauti na maeneo ya kwetu ambao wana jukumu la kushirikiana nasi katika shida na raha. Suala la kwenda kwenye misiba maeneo yote, kwa maana ya Iringa (Nduli, Irore, Kidamali, Magubike, Mufindi, Kalenga, Igominyi, Ilula na kwingineko ambako ndugu wanaishi) ni muhimu sana kwa kila ndugu/mwanaukoo.

Mwenyekiti alisisitiza umuhimu wa kuwatambua wanaukoo wote na kuwashirikisha. Pia alipendekeza vikao vya Wanaukoo vitakavyofanyika mwaka huu 2023, ndugu/wanaukoo waelezwe wazi umuhimu wa kushiriki katika matatizo ya ukoo. Hata wale ambao tayari wana vikundi vyao watueleze wazi kuwa wao wataendelea kushiriki kupitia vikundi vyao…au watashiriki pande zote. Hili ni eneo ambalo pia litakuwa sehemu ya mjadala. Tunaomba ushiriki wa ndugu/wanaukoo uwe mkubwa.

Kikao kwa upande wa Dar es Salaam kimepangwa kufanyika mwaka 2023….Onesmo Bernard Kivenule atatupatia mwongozo wa wapi kikao kitafanyika.  

Kifupi ni haya ambayo yamekuwa sehemu ya mujadala.

Nawasilisha.

Asante

Imetolewa Oktoba 2023

NEMBO YA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE - KAUKI