Chimbuko la Ukoo = KAUKI

Chimbuko la Ukoo = KAUKI
KAUKI

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)
TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA 14 WA KAUKI

Jumatano, 28 Mei 2025

MIKUTANO YA KAUKI

 

1.1.1.            Historia Ya KAUKI

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), ulianzishwa rasmi tarehe 18 Desemba 2005 wakati wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa KAUKI uliofanyika Kijijini Kidamali. KAUKI ilianzishwa kutokana na mashauriano ya Ndugu watatu, yaani Faustino Sigatambule Kivenule, Christian John Kivenule na Adam Alphonce Kivenule.

Ndugu hawa watatu baada ya kubaini mapungufu katika Nyanja ya Mahusiano, Ushirikiano na Kufahamiana miongoni mwa ndugu na wanaukoo kwa ujumla ndani ya Ukoo wa Kivenule, waliamua kuungunisha nguvu zao na kisha kuushirikisha ukoo kuhusiana na adhima yao ya kutaka kuirudisha jamii ya ukoo wa Kivenule kuwa pamoja.

1.1.2.            Mikutano ya Mashauriano

Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mashauriano ulifanyika Jijini Dar es Salaam, mnamo tarehe 06 Februari 2005 katika Ukumbi wa Riverside uliopo eneo la Ubungo, ambapo ndugu zaidi ya 15 walihudhuria. Matokeo ya Kikao hiki yaliazimia kwa kauli moja, kulishirikisha wazo la kuandaliwa kwa MKUTANO MKUU WA KWANZA WA UKOO WA KIVENULE, kwa ndugu zao wanaoishi maeneo ya Magubike, Kidamali, Nyamihuu, Ilalasimba, Idete, Ibogo, Nzihi na Iringa Mjini.

 

Kukubalika kwa wazo hili ndiko kulikopelekea kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule, mnamo tarehe 17 -18 Desemba 2005, Kijijini Kidamali, Mkoani Iringa.

1.1.3.            Idadi ya Mikutano ya KAUKI iliyokwishafanyika

Mara baada ya kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule, pamekuwepo na mwendelezo wa kuendelea kufanyika kwa mikutano hiyo. Tokea wakati huo, Mikutano ya KAUKI imekuwa ikifanyika kila mwaka kwa kuzingatia maeneo ya Kanda. Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa, Mikutano 12 ya KAUKI imefanyika maeneo mbalimbali ya Kanda za KAUKI kama inaoneshwa hapa chini:

1.    Kanda ya Kidamali – Mikutano ya KAUKI 5

2.    Kanda ya Magubike – Mikutano 2

3.    Kanda ya Irore – Mkutano 2 na Mkutano 1 ukiwa umefanyika eneo la Vilalo

4.    Kanda ya Nduli – Mkutano 1

5.    Kanda ya Mufindi – Mkutano 1

6.    Kanda ya Dar es Salaam – Mkutano 1

Kwa KAUKI haya ni matokeo ya Kujivunia kwa sababu siyo rahisi kufanyika kwa mikutano ya namna kutokana na kuandaliwa kwa gharama kubwa.

1.1.4.            Mafanikio Ya KAUKI

KAUKI imefanikiwa kufanya yafuatayo kwa maendeleo ya wana-ukoo. Kwa mfano, Imeanzisha Blogu zake kwa ajili ya upashanaji habari. Anuani za blogu hizo ni:

https://tagumtwa-kivenule.blogspot.com/

https://adamkivenule.blogspot.com/2013/

http://www.kauki-kauki.blogspot.com/

Pia ukiingia kwenye ukurasa wa Google unaweza kuandika Chimbuko na Historia ya Ukoo wa Kivenule au Kuandika neno Kivenule tu…utapata taarifa za kutosha za Ukoo wa Kivenule, zikiwemo blogs na YOUTUBE.

Hali kadhalika, blogu inayomilikiwa na ndugu Adam Kivenule, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa KAUKI imekuwa ikisaidia katika suala nzima usambazaji na upashanaji wa habari za KAUKI. Anuani ya blogu hiyo ni:

https://adamkivenule.blogspot.com/

KAUKI pia imefanikiwa kufungua Ukurasa wa Facebook wenye anuani ifuatayo:

https://www.facebook.com/kivenule/

KAUKI pia imefungua ukurasa wa TWITTER http://www.twitter.com/kivenule

 

Taarifa za KAUKI zipo YOUTUBE unaweza kuingia Youtube na kuandika Ukoo wa Kivenule au Kuandika TAGUMTWA.

Hali kadhalika, unaweza kuwasiliana na viongozi wa KAUKI au ofisi ya KAUKI kwa kutumia baruapepe zifuatazo:

kauki2006@gmail.com

tagumtwa@gmail.com

tagumtwa.kauki@gmail.com

kivenule@gmail.com

Au unaweza kutuma taarifa kuhusiana na ukoo wa Kivenule moja kwa moja kwenye Blog yetu ya Tagumtwa-Kivenule kwa kutumia barua-pepe ifuatayo:

tagumtwa.kauki@blogger.com

 

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni