Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) kwa niaba ya wanaukoo wa Kivenule, unasikitika kutangaza kifo cha Mzee BERNARD HUSSEIN KIVENULE (MNYAMLAFU) kilichotokea Tarehe 21 JUNI 2026, katika Hospitali ya Jeshi Lugalo - Jijini Dar es Salaam.
Taratibu za Mazishi yanaendelea kufanyika nyumbani kwa watoto marehemu MATOSA kwa BONDIA - GOBA, Jijini Dar es Salaam.
Mzee Bernard Hussein Kivenule atakumbukwa kwa mchango wako mkubwa katika kuipigania KAUKI na Mikutano yote ya Ukoo. Amekuwa mstari wa mbele katika kuhimiza umoja wa ukoo wa Kivenule.
Hakuwahi kukosa kushiriki mikutano ya Ukoo iliyofanyika Kidamali na Magubike na maeneo mengine.
Mwenyezi Mungu ailaze, roho ya marehemu mahali pema peponi.
Bwana Alitoa na Sasa ametwaa Jina lake lihimidiwe. Amina
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni