Chimbuko la Ukoo = KAUKI

Chimbuko la Ukoo = KAUKI
KAUKI

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)
TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA 14 WA KAUKI

Jumatatu, 26 Mei 2025

RATIBA YA MKUTANO MKUU WA 14 WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)


https://tagumtwa-kivenule.blogspot.com/

RATIBA YA MKUTANO MKUU WA 14 WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)-KIDAMALI - IRINGA

Siku ya Kwanza: JUMAMOSI  21 JUNI 2024

MUDA

SHUGHULI/JUKUMU

MHUSIKA

12.00-01.00 Asb.

Kuamka na Kujiandaa

Ndugu/Wanaukoo Wote

01.00-02.00

Kupata Kifungua Kinywa (Chai/Kahawa/Uji)

·         Ndugu Wote

·         Kamati ya Maandalizi

02:00-02:50

1.      Kukaribisha Wageni

2.      Kujisajili/Orodhesha Washiriki

3.      Kuwapa Vitambulisho

·         Kamati ya Maandalizi

·         Washiriki Wote

02:50-02:55

Dua/Sala ya Kuombea Mkutano

·         Viongozi wa Dini

02:55-03:00

Salaam toka Kanda ya Kidamali: Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu 14 wa KAUKI

·         Mwakilishi Kanda ya Kidamali

03.00–03.05

Neno fupi la Kumkaribisha na Kumtambulisha Mgeni Rasmi

·         Mwenyekiti wa KAUKI

03.05-03.25

Hotuba ya Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI

·         Mgeni Rasmi

03.25-04.00

Utambulisho wa Ndugu na Wageni Waalikuwa

·         Mwenyekiti-KAUKI

·         Washiriki Wote

04.00-05:00

MADA: Chimbuko/Asili Na Historia Ya Ukoo Wa Kivenule

1.      Mjadala: Muundo wa Ukoo wa Ukoo wa Kivenule (Nakala Zisambazwe)

·         Mtoa Mada

·         Viongozi-KAUKI

·         Washiriki wote

05:00-05:30

Pumziko la Chai / Kahawa/Maji

Washiriki Wote

05.30-07.00

Mchana

Mada Inaendelea

2.      Namna ya Kuiboresha Mada: Mapendekezo

3.      Nini kifanyike kutunza kumbukumbu za Ukoo

4.      Njia Mbadala za Kutunza Taarifa za Ukoo

·         Viongozi-KAUKI

·         Wawezeshaji

·         Washiriki wote

Majumuisho

·         Viongozi wa KAUKI

07.00-08.00

CHAKULA CHA MCHANA

Washiriki wote

08:00-08:40

UCHAGUZI WA VIONGOZI WA KANDA

Nafasi:

1.      Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti

2.      Katibu na Naibu Katibu

3.      Mweka Hazina/ Walezi wa Kanda, Wahamasishaji

1.      Kanda ya DAR

2.      Kidamali/Magubike

3.      Kalenga/Irore

4.      Nduli/Morogoro

5.      Dodoma/Mafinga

08.40 – 09.20

Alasiri

Maendeleo ya KAUKI Katika Kanda:

1.      Hamasa, Mafanikio

2.      Changamoto na Mikakati

·         Viongozi wa Kanda

·         Ndugu toka Kanda Husika

9:20 – 9:45

Hali ya Ukoo/KAUKI: Maendeleo kwa Ujumla;Changamoto;Ushauri na Mapendekezo

·         Viongozi wa KAUKI

·         Wanaukoo Wote

09:45-10:00

Salaam mbalimbali kwenye Mkutano Mkuu 14 wa KAUKI (Wastani watu 6 @ dakika 2)

·         Washiriki wa Mkutano

10.00-10.45

Jioni

Kuahirisha  Mkutano hadi

Siku ya Jumapili tarehe 21 Juni 2025

·         Mwenyekiti – KAUKI

·         Washiriki Wote

02:00 - 06:00   

Usiku

NDUGU KUJUMUIKA PAMOJA (KAUKI NIGHT GALA) kwa ajili ya Vinywaji na Nyama Choma

Ndugu Wote

Kamati ya Maandalizi

   

RATIBA YA MKUTANO MKUU WA 14 WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)-KIDAMALI - IRINGA

Siku ya Pili: JUMAPILI  22 JUNI 2024

MUDA

SHUGHULI/JUKUMU

MHUSIKA

12.00-01.00 Asb.

Kuamka na Kujiandaa kwenda Kanisani

Ndugu Wote

04.00-05.00

Kupata Kifungua Kinywa (Chai/Kahawa/Uji)

·         Ndugu Wote

·         Kamati ya Maandalizi

05:00-06:00

MADA YA II: ELIMU YA UJASILIAMALI - 1

·         Uwasilishaji

·         Mjadala

·         Majumuisho

·         Mwezeshaji

·         Washiriki Wote

06:00-07:00

MADA YA III: ELIMU YA UJASILIAMALI - 2

·         Uwasilishaji

·         Mjadala

·         Majumuisho

·         Mwezeshaji

·         Washiriki Wote

07:00-08:00

MAPUMZIKO YA CHAKULA CHA MCHANA

·         Washiriki Wote

08.00–09.00

Alasiri

MADA YA IV: ELIMU YA UJASILIAMALI - 3

·         Uwasilishaji

·         Mjadala

·         Majumuisho

·         Mwezeshaji

·         Washiriki Wote

09.00-09.30

·         Majumuisho ya Mkutano Mkuu wa 14 wa KAUKI

·         Maazimio

·         Viongozi wa KAUKI

·         Washiriki Wote

09.30-09.40

·         Neo la Shukrani Toka Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 14 wa KAUkI - Kanda Ya Kidamali

·         Mwenyekiti  wa Kamati ya Maandalizi

09.40-09:50

Neno la Shukrani toka kwa Viongozi wa KAUKI

·         Viongozi wa KAUKI

09:50-09:55

KUTANGAZA TAREHE YA MKUTANO MKUU WA 15 WA KAUKI NA MAHALI UTAKAPOFANYIKIA

·         Mwenyekiti – KAUKI

·         Washiriki Wote

09:55.00-10.00

Jioni

Kuahirisha  Mkutano Mkuu wa KAUKI  - 2025

·         Mwenyekiti – KAUKI

 

10:00

MWISHO

Ndugu Wote

Kamati ya Maandalizi

 


Jumatatu, 4 Novemba 2024

CHIMBUKO NA HISTORIA YA UKOO WA KIVENULE

Utangulizi

Mada ya Chimbuko na Historia ya Ukoo wa Kivenule (KAUKI) iliwasilishwa na Mzee William Sigatambule Kivenule. Mwasilishaji wa Mada ni Mzee wa Heshima katika Ukoo wa Kivenule ni Tunu kwa sababu ana madini ya kutosha kuhusiana na masuala ya Ukoo wa Kivenule. KAUKI imekuwa ikimtumia katika Mikutano yake Kuwasilisha Mada ya Chimbuko na Historia ya Ukoo wa Kivenule.

Katika Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI, Mzee Wiliam Sigatambule Kivenule aliwasilisha Mada ya Chimbuko na Historia ya Ukoo wa Kivenule.  Mwasilishaji wa Mada alianza kwa kuelezea kwa kina Chimbuko na Historia ya Ukoo wa Kivenule; huku akielezea kwa kina waanzilishi wa Ukoo wa Mwibalama. Mtoa Mada alisema kuwa Ukoo wa Kivenule awali haukuitwa hivyo, uliitwa MWIBALAMA. Kivenule kwa Asili ni akina Balama ni ndugu wa Karibu kabisa ambao hawapaswi hata kuoana.

Picha ya Mzee William Sigatambule Kivenule wa kwanza kutoka kushoto ndiye aliyewasilisha Mada ya Chimbuko la Ukoo wa Kivenule katika Mkutano Mkuu wa KAUKI (2024)

CHIMBUKO LA UKOO WA KIVENULE

Historia ya Chimbuko la Ukoo wa Kivenule limetoka mbali zaidi hata kabla ya Jina la sasa la KIVENULE kupatikana. Utafiti unaoendelea kufanyika kila mwaka umesaidia kuboresha Chimbuko la Ukoo wa Kivenule.









Picha inaonesha Vitabu vya Chimbuko na Muundo wa Ukoo wa Kivenule vilivyoganywa wakati wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI – Kidamali, Iringa 29 – 30 Juni 2024

Chanzo: KAUKI - 2024

Waanzilishi Sita (6) wa Ukoo wa BALAMA (MWIBALAMA)

Kwa mujibu wa Mzee Wiliam Sigatambule Kivenule, wapo Watoto Sita ndio waliopelekea kuanzishwa kwa Ukoo wa Balama. Vizazi hivyo vya akina Balama vilikuja Kumzaa Tagumtwa BALAMA ambaye baadaye ndiye aliyeleta ukoo wa Kivenule. Chimbuko la Mwibalama ni pale Malangali ambayo ipo Kusini mwa Mufindi, katika Mkoa wa Iringa.

Tafiti za sasa zilizopatikana kupitia Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI zinaonesha kuwa BABU------------- ndiye aliyemzaa BABU MWIGINGILI BALAMA; BABU MWIGINGILI BALAMA ndiye alimzaa BABU MNYARUNGEMBA BALAMA; BABU MNYARUNGEMBA BALAMA ndiye aliyemzaa BABU NYAKUDILA BALAMA; BABU NYAKUDILA BALAMA ndiye aliyemzaa BABU KANOLO BALAMA;  BABU KANOLO BALAMA ndiye aliyemzaa BABU MTENGILINGOMA BALAMA; na BABU MTENGILINGOMA BALAMA akamzaa BABU TAGUMTWA BALAMA.























Picha 2: hazina ya Mashangazi (Sekivenule) kama ilivyochukuliwa katika moja ya matukio yaliyowakutanisha Wanaukoo. Wa pili toka kushoto ni Katibu Mkuu wa Ukoo wa KivenuleChanzo: KAUKI - 2024 

Mababu wote hawa tunaowazungumza hapa chini ni Waanzilishi wa UKOO WA BALAMA (akina MWIBALAMA) na Baadaye UKOO WA KIVENULE.





Maelezo haya yote tunayoyazungumzia ni katika Karne ya 17 kabla ya kuja kwa BABU TAGUMTWA BALAMA, ambaye aliuleta Jina la KIVENULE. BABU MTENGELINGOMA BALAMA ndiye Baba Mzazi wa TAGUMTWA BALAMA.

Wakati huu Babu Tagumtwa Balama alikuwa hajaenda kwenye Vita za LIGALU.




Jumamosi, 28 Septemba 2024

TANZIA

 


TANZIA

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) unasikitika kutangaza kifo cha Mareh. ANNA VANULICHUMA NONGELE, kilichotokea katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili mnano tarehe 06 Septemba 2024, Jijini Dar es Salaam. Mareh. ANNA VANULICHUMA NONGELE ni Mama Mzazi wa Mwenyekiti wa Ukoo Ndugu Onesmo Bernard Kivenule.

Mazishi ya Mareh. ANNA VANULICHUMA NONGELE yamefanyika tarehe 08 Septemba 2024 Kijijini Magubike, Wilaya ya Iringa Vijijini katika Mkoa wa Iringa.

Mareh. ANNA VANULICHUMA NONGELE amekuwa akisumbuliwa na tatizo la Saratani toka mwezi Septemba 2023 na amekuwa akiendelea na matibabu mpaka mauti yalipomfika. Raha ya Milele Umpe Ee Bwana na Mwanga wa Milele umwangazie, apumzike kwa amani – Amina.

Mungu alitoa na leo ametwaa Jina lake Lihimidiwe. Amina.

 

Imetolewa na:

 

Adam Alphonce Kivenule

Katibu Mkuu wa KAUKI