Chimbuko la Ukoo = KAUKI

Chimbuko la Ukoo = KAUKI
KAUKI

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)
TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA 14 WA KAUKI

Jumatano, 28 Mei 2025

MATUKIO KATIKA VIDEO - HUU ULIKUWA MCHANGO WA MWANAUKOO KATIKA MJADALA WA MADA ILIYOWASILISHWA KATIKA MKUTANO WA 13 WA KAUKI


 

MATUKIO YA VIDEO - MKUTANO MKUU WA 13 WA KAUKI - KIDAMALI 2024

 

MIKUTANO YA KAUKI

 

1.1.1.            Historia Ya KAUKI

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), ulianzishwa rasmi tarehe 18 Desemba 2005 wakati wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa KAUKI uliofanyika Kijijini Kidamali. KAUKI ilianzishwa kutokana na mashauriano ya Ndugu watatu, yaani Faustino Sigatambule Kivenule, Christian John Kivenule na Adam Alphonce Kivenule.

Ndugu hawa watatu baada ya kubaini mapungufu katika Nyanja ya Mahusiano, Ushirikiano na Kufahamiana miongoni mwa ndugu na wanaukoo kwa ujumla ndani ya Ukoo wa Kivenule, waliamua kuungunisha nguvu zao na kisha kuushirikisha ukoo kuhusiana na adhima yao ya kutaka kuirudisha jamii ya ukoo wa Kivenule kuwa pamoja.

1.1.2.            Mikutano ya Mashauriano

Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mashauriano ulifanyika Jijini Dar es Salaam, mnamo tarehe 06 Februari 2005 katika Ukumbi wa Riverside uliopo eneo la Ubungo, ambapo ndugu zaidi ya 15 walihudhuria. Matokeo ya Kikao hiki yaliazimia kwa kauli moja, kulishirikisha wazo la kuandaliwa kwa MKUTANO MKUU WA KWANZA WA UKOO WA KIVENULE, kwa ndugu zao wanaoishi maeneo ya Magubike, Kidamali, Nyamihuu, Ilalasimba, Idete, Ibogo, Nzihi na Iringa Mjini.

 

Kukubalika kwa wazo hili ndiko kulikopelekea kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule, mnamo tarehe 17 -18 Desemba 2005, Kijijini Kidamali, Mkoani Iringa.

1.1.3.            Idadi ya Mikutano ya KAUKI iliyokwishafanyika

Mara baada ya kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule, pamekuwepo na mwendelezo wa kuendelea kufanyika kwa mikutano hiyo. Tokea wakati huo, Mikutano ya KAUKI imekuwa ikifanyika kila mwaka kwa kuzingatia maeneo ya Kanda. Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa, Mikutano 12 ya KAUKI imefanyika maeneo mbalimbali ya Kanda za KAUKI kama inaoneshwa hapa chini:

1.    Kanda ya Kidamali – Mikutano ya KAUKI 5

2.    Kanda ya Magubike – Mikutano 2

3.    Kanda ya Irore – Mkutano 2 na Mkutano 1 ukiwa umefanyika eneo la Vilalo

4.    Kanda ya Nduli – Mkutano 1

5.    Kanda ya Mufindi – Mkutano 1

6.    Kanda ya Dar es Salaam – Mkutano 1

Kwa KAUKI haya ni matokeo ya Kujivunia kwa sababu siyo rahisi kufanyika kwa mikutano ya namna kutokana na kuandaliwa kwa gharama kubwa.

1.1.4.            Mafanikio Ya KAUKI

KAUKI imefanikiwa kufanya yafuatayo kwa maendeleo ya wana-ukoo. Kwa mfano, Imeanzisha Blogu zake kwa ajili ya upashanaji habari. Anuani za blogu hizo ni:

https://tagumtwa-kivenule.blogspot.com/

https://adamkivenule.blogspot.com/2013/

http://www.kauki-kauki.blogspot.com/

Pia ukiingia kwenye ukurasa wa Google unaweza kuandika Chimbuko na Historia ya Ukoo wa Kivenule au Kuandika neno Kivenule tu…utapata taarifa za kutosha za Ukoo wa Kivenule, zikiwemo blogs na YOUTUBE.

Hali kadhalika, blogu inayomilikiwa na ndugu Adam Kivenule, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa KAUKI imekuwa ikisaidia katika suala nzima usambazaji na upashanaji wa habari za KAUKI. Anuani ya blogu hiyo ni:

https://adamkivenule.blogspot.com/

KAUKI pia imefanikiwa kufungua Ukurasa wa Facebook wenye anuani ifuatayo:

https://www.facebook.com/kivenule/

KAUKI pia imefungua ukurasa wa TWITTER http://www.twitter.com/kivenule

 

Taarifa za KAUKI zipo YOUTUBE unaweza kuingia Youtube na kuandika Ukoo wa Kivenule au Kuandika TAGUMTWA.

Hali kadhalika, unaweza kuwasiliana na viongozi wa KAUKI au ofisi ya KAUKI kwa kutumia baruapepe zifuatazo:

kauki2006@gmail.com

tagumtwa@gmail.com

tagumtwa.kauki@gmail.com

kivenule@gmail.com

Au unaweza kutuma taarifa kuhusiana na ukoo wa Kivenule moja kwa moja kwenye Blog yetu ya Tagumtwa-Kivenule kwa kutumia barua-pepe ifuatayo:

tagumtwa.kauki@blogger.com

 

 

Jumatatu, 26 Mei 2025

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA WAKATI WA MKUTANO MKUU WA 13 WA KAUKI - KIDAMALI, IRINGA 2024

 

Picha inaonesha Ukumbi uliotumika katika Mkutano Mkuu wa 13 wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI)

Mzee William Sigatambule Kivenule (kushoto) akiwa na Bi. Happy Xavery Kivenule wakati wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI

Wanaukoo mbalimbali wakipata chakula wakati wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI - 2024

Mwenyekiti wa KAUKI akiwa na Mzee William Sigatambule Kivenule ambaye amekuwa akitoa Mada ya Chimbuko na Historia ya Ukoo wa Kivenule

Wanaukoo wakiwa katika Usiku Maalum wa KAUKI - Kidamali Iringa. Hii ilikuwa ni wakati wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI

Bango kuonesha Kaulimbiu ya Ukoo wa Kivenule iliyozinduliwa katika Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI

V
Wanaukoo wakiwa katika Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI uliofanyika Kijijini Kidamali - Iringa Vijijini

Shangazi Anyesi Sigatambule Kivenule kutoka Kanda ya Magubike, naye alikuwa sehemu ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI



Wanaukoo wakiwa tayari kuingia kwenye Mkutano wa 13 wa KAUKI

Wanaukoo wakibadilisha mawazo wakati wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI

Picha ya Kumbukumbu ya Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI. Hawa ni baadhi ya wanaukoo waliohudhuria Mkutano huo.



RATIBA YA MKUTANO MKUU WA 14 WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)


https://tagumtwa-kivenule.blogspot.com/

RATIBA YA MKUTANO MKUU WA 14 WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)-KIDAMALI - IRINGA

Siku ya Kwanza: JUMAMOSI  21 JUNI 2024

MUDA

SHUGHULI/JUKUMU

MHUSIKA

12.00-01.00 Asb.

Kuamka na Kujiandaa

Ndugu/Wanaukoo Wote

01.00-02.00

Kupata Kifungua Kinywa (Chai/Kahawa/Uji)

·         Ndugu Wote

·         Kamati ya Maandalizi

02:00-02:50

1.      Kukaribisha Wageni

2.      Kujisajili/Orodhesha Washiriki

3.      Kuwapa Vitambulisho

·         Kamati ya Maandalizi

·         Washiriki Wote

02:50-02:55

Dua/Sala ya Kuombea Mkutano

·         Viongozi wa Dini

02:55-03:00

Salaam toka Kanda ya Kidamali: Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu 14 wa KAUKI

·         Mwakilishi Kanda ya Kidamali

03.00–03.05

Neno fupi la Kumkaribisha na Kumtambulisha Mgeni Rasmi

·         Mwenyekiti wa KAUKI

03.05-03.25

Hotuba ya Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI

·         Mgeni Rasmi

03.25-04.00

Utambulisho wa Ndugu na Wageni Waalikuwa

·         Mwenyekiti-KAUKI

·         Washiriki Wote

04.00-05:00

MADA: Chimbuko/Asili Na Historia Ya Ukoo Wa Kivenule

1.      Mjadala: Muundo wa Ukoo wa Ukoo wa Kivenule (Nakala Zisambazwe)

·         Mtoa Mada

·         Viongozi-KAUKI

·         Washiriki wote

05:00-05:30

Pumziko la Chai / Kahawa/Maji

Washiriki Wote

05.30-07.00

Mchana

Mada Inaendelea

2.      Namna ya Kuiboresha Mada: Mapendekezo

3.      Nini kifanyike kutunza kumbukumbu za Ukoo

4.      Njia Mbadala za Kutunza Taarifa za Ukoo

·         Viongozi-KAUKI

·         Wawezeshaji

·         Washiriki wote

Majumuisho

·         Viongozi wa KAUKI

07.00-08.00

CHAKULA CHA MCHANA

Washiriki wote

08:00-08:40

UCHAGUZI WA VIONGOZI WA KANDA

Nafasi:

1.      Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti

2.      Katibu na Naibu Katibu

3.      Mweka Hazina/ Walezi wa Kanda, Wahamasishaji

1.      Kanda ya DAR

2.      Kidamali/Magubike

3.      Kalenga/Irore

4.      Nduli/Morogoro

5.      Dodoma/Mafinga

08.40 – 09.20

Alasiri

Maendeleo ya KAUKI Katika Kanda:

1.      Hamasa, Mafanikio

2.      Changamoto na Mikakati

·         Viongozi wa Kanda

·         Ndugu toka Kanda Husika

9:20 – 9:45

Hali ya Ukoo/KAUKI: Maendeleo kwa Ujumla;Changamoto;Ushauri na Mapendekezo

·         Viongozi wa KAUKI

·         Wanaukoo Wote

09:45-10:00

Salaam mbalimbali kwenye Mkutano Mkuu 14 wa KAUKI (Wastani watu 6 @ dakika 2)

·         Washiriki wa Mkutano

10.00-10.45

Jioni

Kuahirisha  Mkutano hadi

Siku ya Jumapili tarehe 21 Juni 2025

·         Mwenyekiti – KAUKI

·         Washiriki Wote

02:00 - 06:00   

Usiku

NDUGU KUJUMUIKA PAMOJA (KAUKI NIGHT GALA) kwa ajili ya Vinywaji na Nyama Choma

Ndugu Wote

Kamati ya Maandalizi

   

RATIBA YA MKUTANO MKUU WA 14 WA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)-KIDAMALI - IRINGA

Siku ya Pili: JUMAPILI  22 JUNI 2024

MUDA

SHUGHULI/JUKUMU

MHUSIKA

12.00-01.00 Asb.

Kuamka na Kujiandaa kwenda Kanisani

Ndugu Wote

04.00-05.00

Kupata Kifungua Kinywa (Chai/Kahawa/Uji)

·         Ndugu Wote

·         Kamati ya Maandalizi

05:00-06:00

MADA YA II: ELIMU YA UJASILIAMALI - 1

·         Uwasilishaji

·         Mjadala

·         Majumuisho

·         Mwezeshaji

·         Washiriki Wote

06:00-07:00

MADA YA III: ELIMU YA UJASILIAMALI - 2

·         Uwasilishaji

·         Mjadala

·         Majumuisho

·         Mwezeshaji

·         Washiriki Wote

07:00-08:00

MAPUMZIKO YA CHAKULA CHA MCHANA

·         Washiriki Wote

08.00–09.00

Alasiri

MADA YA IV: ELIMU YA UJASILIAMALI - 3

·         Uwasilishaji

·         Mjadala

·         Majumuisho

·         Mwezeshaji

·         Washiriki Wote

09.00-09.30

·         Majumuisho ya Mkutano Mkuu wa 14 wa KAUKI

·         Maazimio

·         Viongozi wa KAUKI

·         Washiriki Wote

09.30-09.40

·         Neo la Shukrani Toka Kamati ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 14 wa KAUkI - Kanda Ya Kidamali

·         Mwenyekiti  wa Kamati ya Maandalizi

09.40-09:50

Neno la Shukrani toka kwa Viongozi wa KAUKI

·         Viongozi wa KAUKI

09:50-09:55

KUTANGAZA TAREHE YA MKUTANO MKUU WA 15 WA KAUKI NA MAHALI UTAKAPOFANYIKIA

·         Mwenyekiti – KAUKI

·         Washiriki Wote

09:55.00-10.00

Jioni

Kuahirisha  Mkutano Mkuu wa KAUKI  - 2025

·         Mwenyekiti – KAUKI

 

10:00

MWISHO

Ndugu Wote

Kamati ya Maandalizi