Chimbuko la Ukoo = KAUKI

Chimbuko la Ukoo = KAUKI
KAUKI

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)
TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA 14 WA KAUKI

Jumapili, 10 Septemba 2023

TAARIFA MUHIMU KWA WANAUKOO WA KIVENULE

 


Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) ulifanya kikao cha dharura cha masaa matatu (3) tarehe 7 Septemba 2023 siku ya Alhamisi, Kijijini Kidamali baada ya kuhitimisha mazishi ya ndugu yetu Steward Edgar Kivenule.

Kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wa UKOO wa Kivenule Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule; na kilihudhuriwa na Wanaukoo wengi waliohudhuria mazishi ya Marehemu Stewart Edgar Kivenule.

Agenda Kuu ya Kikao hicho ilikuwa ni kujadili changamoto zilizosababisha kutoendelea kufanyika kwa Mikutano ya UKOO. (Taarifa Rasmi itatolewa).

Aidha UKOO wa Kivenule kupitia Mkutano huu umeazimia kwa Pamoja kuendelea kufanya Mikutano ya UKOO wa Kivenule.

Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Kivenule ujao umepangwa kufanyika Tarehe 29 ya Juni 2024 Kijijini Kidamali. Lengo la kufanyika Kidamali ni kuendelea kuongeza hamasa kwa Wanaukoo wote, na hasa ikizingatiwa kuwa Kidamali kuna mkusanyiko mkubwa wa ndugu.

Kabla ya kufanyika kwa Mkutano huo, kutakuwa na Vikao vya Utangulizi kwa Viongozi wa Kanda mbalimbali ili kuweza kuwasilisha taarifa na pia kuweka mikakati ya kufanikisha Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Mwaka 2024.

Imetolewa na Uongozi wa KAUKI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni