Chimbuko la Ukoo = KAUKI

Chimbuko la Ukoo = KAUKI
KAUKI

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)
TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA 14 WA KAUKI

Jumatatu, 25 Septemba 2023

MIKUTANO YA KANDA YA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)



Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) ulifanya Mkutano wa DHARURA siku ya Alhamisi ya Tarehe 7 Septemba 2023 Kijijini Kidamali kwa Lengo la kuhimiza Wanaukoo wa Kivenule kuendelea kufanya Mikutano ya UKOO. Mkutano huo wa dharura uliofanyika baada ya mazishi ya Marehemu Stewart Edgar Kivenule.

Pamoja na Mambo mengine, Wanaukoo walipendekeza Tarehe ya Mkutano Mkuu wa Ukoo ambao utafanyika Tarehe 29 Juni 2024, Kijijini Kidamali, Mkoani Iringa.

Aidha Viongozi wa Kanda mbalimbali waliombwa kufanya Mikutano ya UKOO ya Kanda ili kuweka mikakati ya kuweza kufanikisha Mkutano huo.

Ikiwa ni Pamoja na kusambaza taarifa na kuweka taratibu za michango kwa ajili ya kufanikisha Mkutano huo.

Imeandaliwa na Umoja wa UKOO wa Kivenule (KAUKI)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni