UTANGULIZI Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) ni sehemu ya harakati za Maendeleo zinazofanywa katika kujikwamua na kuondokana na matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii hii. KAUKI hufanya mikutano kwa wanaukoo kama sehemu wa mwendelezo wa jitihada za namna hii ambayo imekuwa ikifanywa mara moja kila mwaka. Kwa mara kwanza katika historia, Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, ulifanyika, tarehe 17 – 18 Desemba 2005, katika Ukumbi wa Sanga, Kijijini Kidamali, mkoani Iringa. Umoja wa Ukoo wa Kivenule ulizinduliwa rasmi mwaka 2006, katika Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo wa Kivenule uliofanyika tarehe 24 – 25 Juni 2006 katika Ukumbi wa Sanga Kijijini Kidamali, Iringa. Kuzinduliwa kwa Umoja wa Ukoo wa Kivenule, kulienda sambamba na uzinduzi wa Mfuko wa Ukoo pamoja na Kuipitisha Rasimu ya Katiba ya Umoja wa Ukoo wa Kivenule na hivyo kuwa Katiba Rasmi. Kuwepo kwa Katiba ya KAUKI kulitoa fursa ya kuanza kwa utekelezaji wa shughuli na mipango mbalimbali ya maendeleo. Pia, pamoja na mambo mengine, katika Mkutano Mkuu wa Pili wa Ukoo, kulifanya uchaguzi wa Viongozi wa Kanda, uchaguzi wa Walezi wa Ukoo na hivyo utendaji rasmi wa KAUKI kuruhusiwa kuanza. |
Hii ni Blog inayomilikiwa na Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), kwa ajili kuwahabarisha Ndugu na Wanaukoo, taarifa mbalimbali kuhusu Ukoo wa Kivenule. KAUKI ilianzishwa tarehe 18 Desemba 2005 kwenye Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule, uliofanyika Kijijini Kidamali, Mkoani Iringa. Shukrani ziwaendee wote walioshiriki kuanzisha KAUKI: Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule, Ndugu Christian John Kivenule na Ndugu Adam Alphonce Kivenule.
Jumatano, 24 Aprili 2024
IJUE HISTORIA YA KAUKI
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni