Chimbuko la Ukoo = KAUKI

Chimbuko la Ukoo = KAUKI
KAUKI

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)
TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA 14 WA KAUKI

Ijumaa, 27 Oktoba 2023

CHIMBUKO NA MUUNDO WA UKOO WA KIVENULE - KAUKI






VIONGOZI WA KAUKI WASISITIZA UMUHIMU WA KUSHIRIKI KATIKA MISIBA YA NDUGU/WANAUKOO

 

Viongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) walifanya mazungumzo kuhusu umuhimu wa ndugu/wanaukoo kushirikiana katika misiba na raha. Katika mazungumzo hayo, Mwenyekiti wa Ukoo wa Kivenule Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule alielezea kuhusu taratibu zinazotumika maeneo mbalimbali kuhusu uratibu na ushiriki katika misiba ya ndugu/wanaukoo.


Mwenyekiti alifafanua kuwa jukumu la kuratibu, kushiriki na kusimamia shughuli za misiba hubebwa na ndugu/wanaukoo waliopo katika eneo ambalo msiba unakuwa umetokea. Ndugu/Wanaukoo toka maeneo mengine, jukumu lao ni kusaidia kufanikisha shughuli za msiba huo. Kwa muktadha huo, hata viwango vya ushiriki katika msiba husika hutofautiana na wahusika waliopo eneo ambako kuna msiba. Lakini bado wajibu wa kuhakikisha shughuli zinazohusiana na msiba zinafanikiwa ni za kila ndugu/mwanaukoo.

Jambo la muhimu kuzingatia ni ushiriki wa ndugu/wanaukoo katika matukio yote ya misiba ya ndugu/wanaukoo; tofauti inayokuwepo ni viwango vya michango ya rambirambi ili kuweza kufanikisha mazishi ya msiba husika.

Kila maeneo wanatenga viwango vya michango ya rambirambi kwa msiba unaokuwa umetokea katika eneo husika. Pia kuna viwango vya michango kwa ajili ya misiba ambayo inakuwa imetokea mbali na maeneo ambayo msiba unakuwa unakuwa umetokea.

Basi tunasisitiza kuwa ni lazima tushiriki katika misiba yote, ila viwango vitatofautiana kwa misiba ambayo inakuwa imetokea maeneo yetu tunayoishi na ile ambayo imetokea maeneo ambayo hatuishi, lakini tuna wajibu wa kushiriki kwa hali na mali.

Hii itasaidia kupunguza mzigo wa michango kwa sababu kuna wakati kunakuwa na mfululizo wa misiba…kitu ambacho kinaweza kuwafanya ndugu washindwe kumudu.

Kwa hiyo, tunaweza kupendekeza viwango vya michango kwa misiba iliyotokea maeneo ya mbalimbali na tunapaswa kutoa rambirambi zetu.

Kwa ndugu wote tunaoishi Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Mafinga, Mwanza na maeneo mengine tunapaswa kutoa rambirambi kwa msiba uliotokea Magubike. Tutoe chochote kwa kadri Mungu atakavyokuwa ametujalia.

Suala la Jingine lilikuwa kwenye mjadala ni ushiriki wa misiba kwa ndugu/wanaukoo. Tulilizungumzia suala la ndugu wengi waliopo Dar es Salaam na maeneo mengine tofauti na maeneo ya kwetu ambao wana jukumu la kushirikiana nasi katika shida na raha. Suala la kwenda kwenye misiba maeneo yote, kwa maana ya Iringa (Nduli, Irore, Kidamali, Magubike, Mufindi, Kalenga, Igominyi, Ilula na kwingineko ambako ndugu wanaishi) ni muhimu sana kwa kila ndugu/mwanaukoo.

Mwenyekiti alisisitiza umuhimu wa kuwatambua wanaukoo wote na kuwashirikisha. Pia alipendekeza vikao vya Wanaukoo vitakavyofanyika mwaka huu 2023, ndugu/wanaukoo waelezwe wazi umuhimu wa kushiriki katika matatizo ya ukoo. Hata wale ambao tayari wana vikundi vyao watueleze wazi kuwa wao wataendelea kushiriki kupitia vikundi vyao…au watashiriki pande zote. Hili ni eneo ambalo pia litakuwa sehemu ya mjadala. Tunaomba ushiriki wa ndugu/wanaukoo uwe mkubwa.

Kikao kwa upande wa Dar es Salaam kimepangwa kufanyika mwaka 2023….Onesmo Bernard Kivenule atatupatia mwongozo wa wapi kikao kitafanyika.  

Kifupi ni haya ambayo yamekuwa sehemu ya mujadala.

Nawasilisha.

Asante

Imetolewa Oktoba 2023

NEMBO YA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE - KAUKI

 


Jumatatu, 2 Oktoba 2023

MATUKIO MUHIMU KATIKA PICHA - UMOJA WA UKOO WA KIVENULE - KAUKI

 Ni picha matukio mbalimbali wakati wa Msiba wa Marehemu Stewart Edgar Kivenule. Hapa ni eneo la Mlafu katika Maziko ya Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI). Tarehe 7 Septemba 2023

Picha za Wajukuu wa Sigatambule Kivenule

Picha za Wajukuu wa Sigatambule Kivenule

Mwenyekiti wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule

                                                     Picha za Wajukuu wa Sigatambule Kivenule

Mabinti wa Babu Sigatambule na Hussein Kivenule wakiwa na Shangazi yao


Baadhi ya Watoto wa Babu Sigatmbule Kivenule kutoka kushoto, wa pili kulia Mtoto wa Babu Hussein Kivenule na Wajukuu wa Sigatambule

Jumatatu, 25 Septemba 2023

MIKUTANO YA KANDA YA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)



Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) ulifanya Mkutano wa DHARURA siku ya Alhamisi ya Tarehe 7 Septemba 2023 Kijijini Kidamali kwa Lengo la kuhimiza Wanaukoo wa Kivenule kuendelea kufanya Mikutano ya UKOO. Mkutano huo wa dharura uliofanyika baada ya mazishi ya Marehemu Stewart Edgar Kivenule.

Pamoja na Mambo mengine, Wanaukoo walipendekeza Tarehe ya Mkutano Mkuu wa Ukoo ambao utafanyika Tarehe 29 Juni 2024, Kijijini Kidamali, Mkoani Iringa.

Aidha Viongozi wa Kanda mbalimbali waliombwa kufanya Mikutano ya UKOO ya Kanda ili kuweka mikakati ya kuweza kufanikisha Mkutano huo.

Ikiwa ni Pamoja na kusambaza taarifa na kuweka taratibu za michango kwa ajili ya kufanikisha Mkutano huo.

Imeandaliwa na Umoja wa UKOO wa Kivenule (KAUKI)

Jumapili, 10 Septemba 2023

TAARIFA MUHIMU KWA WANAUKOO WA KIVENULE

 


Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) ulifanya kikao cha dharura cha masaa matatu (3) tarehe 7 Septemba 2023 siku ya Alhamisi, Kijijini Kidamali baada ya kuhitimisha mazishi ya ndugu yetu Steward Edgar Kivenule.

Kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wa UKOO wa Kivenule Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule; na kilihudhuriwa na Wanaukoo wengi waliohudhuria mazishi ya Marehemu Stewart Edgar Kivenule.

Agenda Kuu ya Kikao hicho ilikuwa ni kujadili changamoto zilizosababisha kutoendelea kufanyika kwa Mikutano ya UKOO. (Taarifa Rasmi itatolewa).

Aidha UKOO wa Kivenule kupitia Mkutano huu umeazimia kwa Pamoja kuendelea kufanya Mikutano ya UKOO wa Kivenule.

Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Kivenule ujao umepangwa kufanyika Tarehe 29 ya Juni 2024 Kijijini Kidamali. Lengo la kufanyika Kidamali ni kuendelea kuongeza hamasa kwa Wanaukoo wote, na hasa ikizingatiwa kuwa Kidamali kuna mkusanyiko mkubwa wa ndugu.

Kabla ya kufanyika kwa Mkutano huo, kutakuwa na Vikao vya Utangulizi kwa Viongozi wa Kanda mbalimbali ili kuweza kuwasilisha taarifa na pia kuweka mikakati ya kufanikisha Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Mwaka 2024.

Imetolewa na Uongozi wa KAUKI