Chimbuko la Ukoo = KAUKI

Chimbuko la Ukoo = KAUKI
KAUKI

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)

UMOJA WA UKOO WA KIVENULE (KAUKI)
TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA 14 WA KAUKI

Jumamosi, 28 Septemba 2024

TANZIA

 


TANZIA

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) unasikitika kutangaza kifo cha Mareh. ANNA VANULICHUMA NONGELE, kilichotokea katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili mnano tarehe 06 Septemba 2024, Jijini Dar es Salaam. Mareh. ANNA VANULICHUMA NONGELE ni Mama Mzazi wa Mwenyekiti wa Ukoo Ndugu Onesmo Bernard Kivenule.

Mazishi ya Mareh. ANNA VANULICHUMA NONGELE yamefanyika tarehe 08 Septemba 2024 Kijijini Magubike, Wilaya ya Iringa Vijijini katika Mkoa wa Iringa.

Mareh. ANNA VANULICHUMA NONGELE amekuwa akisumbuliwa na tatizo la Saratani toka mwezi Septemba 2023 na amekuwa akiendelea na matibabu mpaka mauti yalipomfika. Raha ya Milele Umpe Ee Bwana na Mwanga wa Milele umwangazie, apumzike kwa amani – Amina.

Mungu alitoa na leo ametwaa Jina lake Lihimidiwe. Amina.

 

Imetolewa na:

 

Adam Alphonce Kivenule

Katibu Mkuu wa KAUKI

Jumapili, 30 Juni 2024

MKUTANO MKUU WA 13 WA KAUKI WAFANYIKA KIDAMALI - IRINGA

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) umefanya Mkutano Mkuu wa 13 katika Kijiji cha Kidamali Mkoani Iringa. Mkutano huo umefanyika mnamo tarehe 29 – 30 Juni 2024, huku ukihudhuriwa na ndugu na wanaukoo zaidi ya 70 wakiwa na Vitambulisho vyao.

Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI unafanyika kwa mara nyingine baada ya Mkutano Mkuu wa Mwisho wa Ukoo wa Kivenule uliofanyika katika Kijiji cha Vilalo, Irore Mkoani Iringa.

Baadhi ya Wanaukoo wa Kivenule waliohudhuria Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI, Kidamali - Iringa


Mahudhurio ya Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI hayakuwa ya Kuridhisha kutokana na baadhi ya Kanda kutokuwa na Uwakilishi. Kanda ya Kidamali, Magubike, Dar eS Salaam, Mafinga, Morogoro, Iringa Mjini na Kalenga ndizo zilizokuwa na Uwakilishi katika Mkutano huo. Kanda za Nduli, Mgongo, Itagutwa, Igominyi na Vilalo hawakuhudhuria Mkutano kwa sababu ambazo hazikuweza kufahamika.

Mojawapo ya mambo makubwa yaliyofanyika katika Mkutano huo ni pamoja na kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa Viongozi wa KAUKI watakaotumikia nafasi zao kwa kipindi cha miaka 3 kwa mujibu wa Katiba ya KAUKI.

Hali kadhalika Mada mbalimbali ziliwasilishwa kwa Wanaukoo zikiwa na lengo la kuwajengea uwezo na pia kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili wanaukoo.

Mkutano wa KAUKI wa 13 pia ulijadili changamoto mbalimbali zinazoukabili ukoo wa Kivenule na namna ya kuweza kuzitatua. Changamoto hizo ni pamoja na migogoro ya ardhi baina ya Ukoo wa Kivenule na Mwekezaji, ambao ulichukua sehemu kubwa ya ardhi. Mgogoro ardhi unaligusa eneo la Ulefi na eneo la Magubike, ambapo haya maeneo yaliyotwaliwa na Mwekezaji yalikuwa chini ya Umiliki wa Ukoo wa Kivenule na hata ushahidi wa Makaburi ya Waasisi wa Ukoo yapo kwenye hiyo ardhi iliyotwaliwa.

Mzee Bernard Hussein Kivenule akiwa na Dada zake wakati wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI - Kidamali Iringa.

Changamoto nyingine kuzorota kwa mahusiano baina ya Wanaukoo na kutofanyika kwa Mikutano ya KAUKI toka mwaka 2017.

Pia Mkutano huo ulikuja na mpango madhubuti wa ukusanyaji wa michango na pia kuendelea kuboresha Mikutano Mikuu ya Ukoo ya Kivenule.

Wanaukoo wote kwa pamoja walikubaliana kwamba wataanza kutumia M-Koba kama njia madhubuti ya Ukusanyaji na Utunzaji wa Fedha za Michango toka kwa Wanaukoo.


Usiku wa Chakula Maalum kwa Wanaukoo - kilichofanyika wakati wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI

Jumla ya Ahadi ya Shilingi Milioni 1,250,000 zilipatikana kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa 14 wa KAUKI, utakaofanyika Kijijini Kidamali. Aidha kiasi cha shilingi 130,000/-  taslimu zilipatikana wakati wa Mkutano huo ikiwa ni michango iliyotokana na ahadi toka kwa Wanaukoo kwa ajili ya Mkutano Mkuu Ujao wa KAUKI.

MABORESHO KATIKA MKUTANO MKUU WA 13 WA KAUKI

Moja ya eneo lililoboreka kwenye Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Kivenule ni kuongezeka kwa Bajeti ya Mkutano na pia Wanaukoo kuwa katika Mavazi rasmi ya Mkutano huo. Wanaukoo wa Kanda ya Dar es Salaam, Dodoma, Mafinga na Morogoro walijitoa kwa hali na Mali kwa lengo la kufanikisha Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI. Hii ndiyo sababu ya kuboreka kwa bajeti ya Mkutano huo.

Mkutano wa 13 wa KAUKI uliandaa Usiku Maalum kwa Wanaukoo – Dinner Night Gala kwa Wanaukoo ambapo walijumuika pamoja, kunywa, kula na kubadilishana mawazo. Hili likuwa ni tukio adhimu ambalo lilikuwa halijawahi kutokea katika Mkutano wowote wa KAUKI.

Wanaukoo wakiwa katika Vazi la Tshirt Maalum zenye Nembo ya KAUKI waliupendezesha Mkutano Mkuu wa 13. Tshirt zenye rangi ya Kijivu, Nyeupe, Bluu na Rangi ya Damu ya Mzee zilivaliwa na Wanaukoo na Kuupamba Mkutano.

Imeandaliwa na:

 

Adam Alphonce Kivenule

Katibu Mkuu - KAUKI

Jumamosi, 29 Juni 2024

UKOO WA KIVENULE WAFANYA UCHAGUZI WA VIONGOZI WAKE

 


KAUKI YAFANYA UCHAGUZI WA VIONGOZI

Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) umefanya Uchaguzi wa Viongozi wake. Uchaguzi huu umefanyika leo Kidamali, Iringa wakati wa Mkutano Mkuu wa 13 wa Ukoo.

Uchaguzi huo umehusisha uchaguzi wa Mwenyekiti wa Ukoo, Makamu wa Mwenyekiti wa Ukoo, Katibu Mkuu wa Ukoo, Makamu wake, Mweka Hazina na Walezi wa KAUKI.

Waliochaguliwa kushika nyadhifa hizo ni pamoja na:

1.    Ndugu Onesmo Bernard Kivenule aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Ukoo

2.    Bi. Gloria Xavery Kivenule ambaye amechaguliwa kuwa Makamu wa Mwenyekiti wa Ukoo

3.    Ndugu Adam Alphonce Kivenule aliyechaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Ukoo,

4.    Ndugu Christian John Kivenule aliyechaguliwa kuwa Katibu Msaidizi

5.    Ndugu Lesandu Peter Mhapa aliyechaguliwa kuwa Mweka Hazina wa Ukoo; na:

Waliochaguliwa kuwa Walezi wa Ukoo Ukoo wa

6.    Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule

7.    Ndugu Vitus Nzala na

8.    Bi. Irene Kivenule  Kivenule.

Jumapili, 23 Juni 2024

DOKOZE KUTOKA UMOJA WA UKOO WA KIVENULE - KAUKI

 

VIONGOZI WA KAUKI WASISITIZA UMUHIMU WA KUSHIRIKI KATIKA MISIBA YA NDUGU/WANAUKOO

Viongozi wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) walifanya mazungumzo kuhusu umuhimu wa ndugu/wanaukoo kushirikiana katika misiba na raha. Katika mazungumzo hayo, Mwenyekiti wa Ukoo wa Kivenule Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule alielezea kuhusu taratibu zinazotumika maeneo mbalimbali kuhusu uratibu na ushiriki katika misiba ya ndugu/wanaukoo.

Mwenyekiti alifafanua kuwa jukumu la kuratibu, kushiriki na kusimamia shughuli za misiba hubebwa na ndugu/wanaukoo waliopo katika eneo ambalo msiba unakuwa umetokea. Ndugu/Wanaukoo toka maeneo mengine, jukumu lao ni kusaidia kufanikisha shughuli za msiba huo. Kwa muktadha huo, hata viwango vya ushiriki katika msiba husika hutofautiana na wahusika waliopo eneo ambako kuna msiba. Lakini bado wajibu wa kuhakikisha shughuli zinazohusiana na msiba zinafanikiwa ni za kila ndugu/mwanaukoo.

Jambo la muhimu kuzingatia ni ushiriki wa ndugu/wanaukoo katika matukio yote ya misiba ya ndugu/wanaukoo; tofauti inayokuwepo ni viwango vya michango ya rambirambi ili kuweza kufanikisha mazishi ya msiba husika.

Kila maeneo wanatenga viwango vya michango ya rambirambi kwa msiba unaokuwa umetokea katika eneo husika. Pia kuna viwango vya michango kwa ajili ya misiba ambayo inakuwa imetokea mbali na maeneo ambayo msiba unakuwa unakuwa umetokea.

Basi tunasisitiza kuwa ni lazima tushiriki katika misiba yote, ila viwango vitatofautiana kwa misiba ambayo inakuwa imetokea maeneo yetu tunayoishi na ile ambayo imetokea maeneo ambayo hatuishi, lakini tuna wajibu wa kushiriki kwa hali na mali.

Hii itasaidia kupunguza mzigo wa michango kwa sababu kuna wakati kunakuwa na mfululizo wa misiba…kitu ambacho kinaweza kuwafanya ndugu washindwe kumudu.

Kwa hiyo, tunaweza kupendekeza viwango vya michango kwa misiba iliyotokea maeneo ya mbalimbali na tunapaswa kutoa rambirambi zetu.

Kwa ndugu wote tunaoishi Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma, Mafinga, Mwanza na maeneo mengine tunapaswa kutoa rambirambi kwa msiba uliotokea Magubike. Tutoe chochote kwa kadri Mungu atakavyokuwa ametujalia.

Suala la Jingine lilikuwa kwenye mjadala ni ushiriki wa misiba kwa ndugu/wanaukoo. Tulilizungumzia suala la ndugu wengi waliopo Dar es Salaam na maeneo mengine tofauti na maeneo ya kwetu ambao wana jukumu la kushirikiana nasi katika shida na raha. Suala la kwenda kwenye misiba maeneo yote, kwa maana ya Iringa (Nduli, Irore, Kidamali, Magubike, Mufindi, Kalenga, Igominyi, Ilula na kwingineko ambako ndugu wanaishi) ni muhimu sana kwa kila ndugu/mwanaukoo.

Mwenyekiti alisisitiza umuhimu wa kuwatambua wanaukoo wote na kuwashirikisha. Pia alipendekeza vikao vya Wanaukoo vitakavyofanyika mwezi huu Oktoba 2023, ndugu/wanaukoo waelezwe wazi umuhimu wa kushiriki katika matatizo ya ukoo. Hata wale ambao tayari wana vikundi vyao watueleze wazi kuwa wao wataendelea kushiriki kupitia vikundi vyao…au watashiriki pande zote. Hili ni eneo ambalo pia litakuwa sehemu ya mjadala. Tunaomba ushiriki wa ndugu/wanaukoo uwe mkubwa.

Kikao kwa upande wa Dar es Salaam kimepangwa kufanyika tarehe 14 Oktoba 2023….Onesmo Bernard Kivenule atatupatia mwongozo wa wapi kikao kitafanyika.  

Kifupi ni haya ambayo yamekuwa sehemu ya mujadala.

Nawasilisha.

Asante

Imetolewa leo tarehe 02 Oktoba 2023

RATIBA YA MKUTANO MKUU WA 13 WA KAUKI - KIDAMALI , IRINGA

 

RATIBA YA SIKU MOJA YA MKUTANO MKUU WA KAUKI

KIDAMALI - IRINGA

29 Juni 2024

MUDA

SHUGHULI/JUKUMU

MHUSIKA

12.00-01.00

Asubuhi

Kuamka na Kujiandaa

Ndugu Wote

01.00-02.00

Kifungua Kinywa (Chai/Kahawa)

Ndugu Wote

02:00-03:00

Kujisajili na Kupata Vitambulisho

Washiriki Wote

03.00–03.15

Hotuba ya Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI

Mwenyekiti wa KAUKI

03.15-03.30

Ufunguzi Rasmi wa Mkutano na Mgeni Rasmi

Mgeni Rasmi

03.30-04.00

Utambulisho wa Ndugu na Wageni Waalikuwa

Washiriki Wote

04.00-05:00

Mada: CHIMBUKO NA HISTORIA YA UKOO

1.      Washiriki wasambaziwe nakala ya muundo wa Ukoo na kasha kuujadili na kutoa mawazo yao

·         Mwakilishi – Kidamali

·         Mwakilishi - Ilole

·         Washiriki wote

05:00-05:30

Pumziko la Chai / Kahawa/Maji

Washiriki Wote

05.30-07.00

Mchana

Mada Inaendelea.

2.      Washiriki waijadili mada na kutoa mapendekezo

3.      Washiriki waijadili mada na kupendekeza nini kifanyike kutunza kumbukumbu hizo

4.      Washiriki wazijadili njia mbadala za kutunza taarifa zinazohusiana na ukoo

Wawezeshaji na Washiriki wote

Majadiliano

Washiriki wote na Wawezeshaji

Majumuisho

Wawezeshaji

07.00-08.00

CHAKULA CHA MCHANA

Washiriki wote

08:00-08:40

TAARIFA YA UTENDAJI WA KAUKI:

1.      Mipango na Shughuli zilizokusudiwa kufanywa na KAUKI 2017-2024;

2.      Taarifa ya Utendaji kwa Ujumla;

3.      Taarifa ya Mahesabu na Fedha; na

4.      Mafanikio na Matatizo ya KAUKI

5.      Matarajio ya KAUKI 2024/25

6.      Changamoto za KAUKI na Namna ya Kukabiliana nazo

1.      Katibu Mkuu

2.      Makamu wa Katibu

3.      Mhasibu

08.40 – 09.20

Alasiri

TAARIFA YA SHUGHULI ZA MAENDELEO KATIKA KANDA

1. HAMASA

2. CHANGAMOTO

3. MIKAKATI

4. MAFANIKIO

·         Viongozi wa Kanda zote

·         Ndugu toka Kanda Husika

9:20 – 9:45

HALI YA UKOO/KAUKI

Kujadili Mapungufu, Kutoa Ushauri, Mapendekezo

·         Katibu Mkuu

·         Katibu Msaidizi

·         Washiriki wote

09:45-10:00

Salaam mbalimbali kutoka kwa Washiriki wa Mkutano Mkuu (Wastani watu 6 na dakika @ 5)

Washiriki wa Mkutano

10.00-10:30

Jioni

Uzoefu wa wanaukoo katika shughuli za maendeleo

1.      Kidamali/Magubike: Kilimo cha Nyanya /Tumbaku na shughuli nyingine za kiuchumi dakika 25

2.      Ilole/Nduli/Kigonzile/Mgongo: Uzoefu wa Shughuli za Kiuchumi dakika 25

3.      Dar/ Morogoro/ Kilombero / Dodoma/Mafinga dakika 5

4.      Maeneo Mengine

Washiriki wote; viongozi wa Kanda au wajumbe watakaochaguliwa kutoa uzoefu wa shughuli hizo za kiuchumi

10.30-10:35

Kutaja Tarehe ya Mkutano Mwingine wa KAUKI

Kuahirisha Mkutano

 

10.35-10.45

KUAHIRISHA MKUTANO

Viongozi wa Dini

Kiongozi wa KAUKI

Mapumziko : Chai/Kahawa/Maji na Vinywaji

Washiriki wote

30 Juni 2024

MUDA

SHUGHULI/JUKUMU

MHUSIKA

12.00-02.00

Asubuhi

Kuamka na Kuhudhuria Ibada (Kanisani)

Ndugu Wote wa Dhehebu la Kikristo

02.00-03.00

Kifungua Kinywa (Chai/Kahawa)

Ndugu Wote

03:00-03:30

Kujisajili na Kupata Vitambulisho

Washiriki Wote

03.30–04.15

MADA:

Mtoa Mada

04.15-04.30

Mjadala Kuhusiana na Mada

Wote

04.30-05.30

MADA:

Mtoa Mada

05.30-06:30

Mchana

MADA:

Mtoa Mada

06.30-07.20

YATOKANAYO NA MKUTANO MKUU

1.      Maazimio ya Mkutano Mkuu wa 13 wa KAUKI

2.      Mipango na Mikakati ya KAUKI

3.      Tarehe ya Mkutano Mkuu wa 14 wa KAUKI

Viongozi

Wanaukoo

Majadiliano

Washiriki wote na Wawezeshaji

Majumuisho

Wawezeshaji

07.20-07.40

SALAAM TOKA KANDA MBALIMBALI

Washiriki wote

07:40-08:00

SALA

KUFUNGA MKUTANO

Viongozi wa Dini

Viongozi wa Ukoo